Monday, June 11, 2012

Jeneza La Marehemu Bob Makani

















                         Mawaziri wafariki ajali ya helikopta




NI PROF SAITOTI, NAIBU WAKE NA MAOFISA WA JUU WA SERIKALI YA KENYA
Mwandishi wetu, Nairobi
WAZIRI wa Usalama wa Ndani Kenya, Profesa George Saitoti na Naibu wake, Orwa Ojode pamoja na maofisa wengine watano, wamefariki dunia baada ya helikopta ya Polisi waliyokuwa wamepanda kuanguka msituni.
Profesa Saitoti ambaye ni mmoja wa mawaziri waandamizi katika Serikali ya Rais Mwai Kibaki na mmoja wa wanasiasa wakongwe wanaoheshimika Kenya, aliwahi pia kuwa Makamu wa Rais kati ya mwaka 1976 hadi 1979 na alishatangaza kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwakani.
Jana, Saitoti ambaye ni mchumi aliyebobea na bingwa hisabati, akiwa na naibu wake na maofisa hao wa wizara walipata ajali wakati wakielekea katika eneo la Sotik kwa ajili ya  mkutano wa usalama.
Ajali hiyo ilitokea asubuhi katika eneo la Kibiku, karibu na Mji wa Ngong, kilometa 20  kutoka Nairobi.
Taarifa zilisema helikopta hiyo ya polisi ilikuwa imebeba abiria saba ambao wote walifariki dunia huku miili yao ikiharibika vibaya.
Profesa Saitoti alikuwa Mbunge wa Kajiado tangu mwaka 1988 hadi mauti yalipomkuta.

Mashuhuda
Walioshuhudia ajali hiyo, walisema waliona helikopta hiyo ikizunguka angani kabla ya kuanguka katika Msitu wa Ngong.
Baada ya kutokea ajali hiyo, polisi walilizingira eneo la ajali huku Kamishna wa Polisi, Mathew Iteere ambaye na yeye alikuwapo katika eneo hilo akisema atatoa taarifa kamili kuhusiana na  ajali hiyo kwa waandishi wa habari baadaye.
Ajali hiyo imetokea ikiwa ni miaka minne tu tangu kutokea kwa ajali nyingine ya helikopta Juni 10, 2008 ambayo ilisababisha vifo vya mawaziri wawili.
Mawaziri walipoteza maisha katika ajali hiyo ni pamoja na Kipkalya Kones na Lorna Laboso.

Mambo muhimu kwa Saitoti
Saitoti ambaye alizaliwa mwaka 1945 kabla ya kupatwa na mauti hayo, aliwahi kutoa wito kwa raia wa Kenya  kuwachagua viongozi ambao ni watendaji wa kazi bila ya kuangalia kabila, rangi na dini.
Kiongozi huyo ambaye kabla ya kuwa Waziri wa Usalama wa Ndani, alikuwa Waziri wa Fedha na pia Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia kati ya mwaka 1990 hadi 2001, alisema Wakenya wanapaswa kuwachunguza viongozi kabla ya kuwachagua ili kuepuka kuchagua wala rushwa.
Profesa Saitoti alibainisha kuwa kuna haja ya wanasiasa wote  kutowagawa Wakenya wakati wa kampeni zao ili kuepuka kile kilichotokea katika uchaguzi 2007.
Alisema kutokana na uzoefu wake, yeye ndiye aliyekuwa na uwezo wa kumrithi Rais Mwai Kibaki.
“Mataifa yote yanatuangalia sisi sasa hivi, nini tunachokifanya wakati huu na nini kitakachotokea wakati wa uchaguzi mkuu mwakani,” alisema.
Marehemu Saitoti ndiye aliyekuwa akiongoza jeshi la nchi hiyo kwa ajali ya kuwatafuta wafuasi wa kundi la Al Shabab, Somalia



MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MAONYESHO YA KWANZA YA TANZANIA HOMES EXPRO

 

 

 

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kuhusu utengenezaji wa Viage vya ujenzi wa Nyumba kutoka kwa Ofisa Masoko wa Kampuni ya Insignia Ltd, Obed Machoka, wakati Makamu alipokuwa akitembelea katika mabanda ya maonyesho ya kwanza ya Tanzania Homes Expro, yaliyofanyika leo Juni 10 katika Viwanja vya Mlimani City Mwenge jijini Dar es Salaam.Picha na Muhidin Sufiani-OMR

 

 



Saturday, June 9, 2012

Marufuku kuuza damu

9th June 2012
                                             Dk. Hussein Mwinyi          
         Serikali imewatahadharisha na kuwakemea wahudumu wa afya wote wenye tabia ya kuuza damu kwa wagonjwa kuwa hatua kali dhidi yao zitachukuliwa.

Aidha hospitali zote zimeagizwa kuweka mabango yanayoonyesha kuwa damu haiuzwi, na wananchi wametakiwa kutoa taarifa kwa viongozi pindi wanapoona wahudumu wanauza damu.

Tadhari hiyo ilitolewa jana na Waziri  Dk. Hussein Mwinyi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakati akitoa tamko la wizara hiyo kuhusu maadhimisho ya siku ya wachangia damu salama duniani ambayo huadhimishwa kila Juni 14 ambapo kitaifa hafla hiyo itafanyika mjini Moshi mkoani Arusha.

"...wizara yangu inakemea na kulaani kitendo cha kuuza damu kwa wagonjwa wakati inapatikana bure kwenye kanda zetu..." alisema na kueleza kuwa kauli mbiu ya mwaka huu ni 'kila mchangia damu ni shujaa'.

Dk. Mwinyi alisema kuwa tangu kuanza kwa mpango wa damu salama nchini 2004, kumekuwa na mafanikio mbalimbali yakiwemo ya ongezeko la vituo vya kanda kutoka vinne mwaka 2006 hadi vinane mwaka 2007.

Mafanikio mengine ameyataja kuwa ni ongezeko la ukusanyaji wa damu kutoka chupa 52,000 mwaka 2005 hadi 140,000 mwaka jana ambapo mahitaji halisi kwa mwaka ni wastani wa kati ya chupa 350,000 na 400,000 ingawa malengo yaliyopo katika kipindi cha mwaka huu na mwaka ujao ni kati ya chupa 180,000 na 200,000.

Alisema mafanikio mengine ni kupungua kwa kiwango cha virusi vya Ukimwi kwenye damu inayokusanywa na vituo vya damu salama kutoka asilimia saba mwaka 2005 hadi asilimia moja mwaka jana na uanzishwaji wa mfumo mpya wa teknolojia ya habari na mawasiliano unaosimamia shughuli zote za upatikanaji wa damu salama.

Hata hivyo, alisema kumekuwepo na changamoto nyingi zikiwemo za mahitaji makubwa ya damu kuliko upatikanaji wake, uelewa mdogo wa jamii kuhusu suala la uchangiaji wa damu kwa hiari, uuzwaji damu usio halali, matumizi yasiyo sahihi ya damu katika hospitali na miundombinu hafifu hasa ya barabara.

Dk. Mwinyi aliziomba taasisi mbalimbali na viongozi wa serikali, siasa, dini na jamii kushirikiana na serikali katika jitihada hizi ili kunusuru maisha ya wahitaji wa damu.

Kuhusu maambukizi ya Ukimwi, alisema takwimu zinaonyesha kuwa asilimia kati ya tano na 10 ya maambukizi hayo husababishwa na mgonjwa kuongezewa damu yenye virusi vya ugonjwa huo ingawa yapo magonjwa mengine kama vile virusi vya homa ya ini na kaswende.

Maadhimisho hayo ambayo kidunia yanaadhimishwa mjini Seoul, Jamhuri ya Korea, madhumuni yake hasa ni kuwashukuru na kuwashawishi wachangiaji damu kujiheshimu ili waendelee kufanya hivyo, kuwatia moyo wasiochangia kufanya hivyo na kuwahimiza wafanyakazi wa huduma za damu kuwatambua wachangiaji.


Wakuu wapya wa wilaya hawana ofisi

SERIKALI  imepoteza zaidi ya Sh5.4 bilioni kutokana na kulipa mishahara kwa wafanyakazi hewa 9,949 katika kipindi cha miezi mitano iliyopita.Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa alisema vitendo hivyo vimekwamisha utekelezaji wa miradi mingine ya maendeleo ambayo ingegharamiwa kwa fedha hizo.

Kauli ya Dk Mgimwa imekuja ikiwa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu Rais Jakaya Kikwete alipotoa agizo la kudhibiti wafanyakazi hewa katika wizara na idara za Serikali.

Machi mwaka jana, Rais Kikwete aliamuru kufanyika kwa ukaguzi katika idara zote za serikali kutokana na kuwapo kwa taarifa kwamba kiasi cha Sh9 bilioni kilikuwa kimelipwa kama mishahara kwa wafanyakazi hewa katika wizara tatu tu za Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Katiba na Sheria na Afya na Ustawi wa Jamii.Rais alisema wahusika wa vitendo hivyo walipaswa kubainishwa ikiwa ni hatua ya kukomesha mara moja wizi wa fedha za umma kupitia mishahara hewa na kwamba Serikali haipaswi kuwaruhusu watu ambao wameiibia Serikali fedha kuendelea kufanya kazi za umma.

Lakini jana akifungua Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha lililofanyika Dar es Salaam, Dk Ngimwa alikiri kuwapo kwa tatizo hilo, mwaka mmoja tangu kutolewa kwa agizo hilo la Rais Kikwete.
Kutokana na hali hiyo, alisema Serikali imechukua hatua za kukabiliana na ufisadi huo kwa kuweka utaratibu wa orodha ya wafanyakazi kupitiwa kila mwezi.Aliwataka wafanyakazi wenye tabia hiyo kuiacha mara moja akisema Serikali iko makini na itawachukulia hatua kali wahusika wote.

Alisema wiki ijayo itasomwa Bajeti ya Serikali 2012/13 ambayo imezingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na imelenga ukuaji wa uchumi wa kiwango cha kati, hivyo suala la udhibiti wa mapato ya Serikali halitakuwa na mjadala.

“Tunataka kuleta hali bora ya maisha ya wananchi. Lengo la Serikali ni kila mmoja kupata wastani wa pato la Dola za Marekani 3,000 (Sh3.8 milioni) kila mwezi ifikapo mwaka 2025,” alisema.
Alisema bila udhibiti wa tatizo la mishahara ya wafanyakazi hewa, ni vigumu kufikia lengo hilo hivyo kuwataka wafanyakazi wa wizara hiyo kujipanga vizuri ili lengo hilo lifikiwe.

Alisema wafanyakazi wa Hazina ndiyo wanaobeba jukumu hilo wakati Serikali inajitahidi kupambana na mtikisiko wa kiuchumi hususan kipindi hiki cha kuelekea bajeti.Alisema Serikali imeomba nguvu ya kujiongezea uwezo kutoka mashirika ya kimataifa, nchi za Mashariki ya Kati na Asia.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, Ramadhan Khijjah alisema kuna tatizo la wafanyakazi wa wizara hiyo kuogopa kuzungumza katika vikao vya baraza hilo.

“Watu waoga huogopa kuzungumza. Wanawahofia wakuu wao wa idara jambo ambalo halijengi,” alisema.
Alisema hali hiyo inachangiwa na walio wengi kuogopa kuchukiwa na mabosi wao jambo ambalo alilipinga na kuwatoa hofu akiwataka wawe wazi.

Alisema mabaraza hayo ndiyo sehemu ya kukosoa, kuelekeza na kubainisha kasoro zilizopo ili hatua zichukuliwe na kujenga mshikamano kwa manufaa ya Taifa na jamii kwa ujumla.
 

DK. Mwakyembe: Nishaonja kifo siogopi kufa

 

 

Waziri wa Uchukuzi, Dk.Harrison Mwakyembe, ameapa kuwa hataogopa vitisho vyovyote kuwafukuza kazi watumishi wa mashirika, taasisi na idara za serikali zilizopo chini ya wizara yake wanaokwenda kinyume cha utendaji kazi kwani kama ni suala la kufa alishaonja kufa kipindi alipougua.

Alisema hayo juzi wakati akizungumza na wafanyakazi wa Chuo cha Bahari kilichopo jijini Dar es Salaam baada ya kukitembelea ikiwa ni siku moja baada kutembelea Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

“Nawahakikishia bandari itanyooka, nitapigana hadi dakika ya mwisho, sitaogopa kufa maana kama ni suala la kufa tayari nilishaonja kufa nilipougua sana,”alisema Dk.Mwakyembe.

Alisema nchi hii haisongi mbele kimaendeleo kutokana na maneno kuwa mengi na kwamba katika ziara yake aliyoifanya katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) amekuta kuna uozo mwingi na kuahidi kusafisha wale wote ambao wanatuhumiwa kuhusika na kashifa mbalimbali bandarini hapo.

Dk.Mwakyembe alisema wakati anachukua hatua za kusafisha kwa kuwang’oa watumishi wabadhirifu katika taasisi, idara, mashirika yaliyopo chini ya Wizara ya Uchukuzi, wanafunzi waliomaliza darasa la saba, kidato cha nne na sita wakae mkao wa kula  kwa ajili ya kuziba nafasi hizo.

“Na katika hili sitanii, hapa nitaomba kabisa wale wanafunzi waliomaliza darasa la saba, kidato cha nne, sita na chuo kikuu waanze kujioorodhesha kabisa majina yao maana nitawafukuza kazi watu wengi sana katika wizara hii,” alisema Dk.Mwakyembe.

Aidha waziri huyo aliutaka uongozi wa Chuo cha Bahari kuwa wawazi kwa wafanyakazi wao kwa kuwaeleza mapato na matumizi ili watumishi wasiwe wanajenga hoja kwamba fedha zao zinaliwa.
 
Serikali yalipa Sh5 bilioni wafanyakazi hewa 10,000
 
SERIKALI  imepoteza zaidi ya Sh5.4 bilioni kutokana na kulipa mishahara kwa wafanyakazi hewa 9,949 katika kipindi cha miezi mitano iliyopita.Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa alisema vitendo hivyo vimekwamisha utekelezaji wa miradi mingine ya maendeleo ambayo ingegharamiwa kwa fedha hizo.

Kauli ya Dk Mgimwa imekuja ikiwa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu Rais Jakaya Kikwete alipotoa agizo la kudhibiti wafanyakazi hewa katika wizara na idara za Serikali.

Machi mwaka jana, Rais Kikwete aliamuru kufanyika kwa ukaguzi katika idara zote za serikali kutokana na kuwapo kwa taarifa kwamba kiasi cha Sh9 bilioni kilikuwa kimelipwa kama mishahara kwa wafanyakazi hewa katika wizara tatu tu za Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Katiba na Sheria na Afya na Ustawi wa Jamii.Rais alisema wahusika wa vitendo hivyo walipaswa kubainishwa ikiwa ni hatua ya kukomesha mara moja wizi wa fedha za umma kupitia mishahara hewa na kwamba Serikali haipaswi kuwaruhusu watu ambao wameiibia Serikali fedha kuendelea kufanya kazi za umma.

Lakini jana akifungua Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha lililofanyika Dar es Salaam, Dk Ngimwa alikiri kuwapo kwa tatizo hilo, mwaka mmoja tangu kutolewa kwa agizo hilo la Rais Kikwete.
Kutokana na hali hiyo, alisema Serikali imechukua hatua za kukabiliana na ufisadi huo kwa kuweka utaratibu wa orodha ya wafanyakazi kupitiwa kila mwezi.Aliwataka wafanyakazi wenye tabia hiyo kuiacha mara moja akisema Serikali iko makini na itawachukulia hatua kali wahusika wote.

Alisema wiki ijayo itasomwa Bajeti ya Serikali 2012/13 ambayo imezingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na imelenga ukuaji wa uchumi wa kiwango cha kati, hivyo suala la udhibiti wa mapato ya Serikali halitakuwa na mjadala.

“Tunataka kuleta hali bora ya maisha ya wananchi. Lengo la Serikali ni kila mmoja kupata wastani wa pato la Dola za Marekani 3,000 (Sh3.8 milioni) kila mwezi ifikapo mwaka 2025,” alisema.
Alisema bila udhibiti wa tatizo la mishahara ya wafanyakazi hewa, ni vigumu kufikia lengo hilo hivyo kuwataka wafanyakazi wa wizara hiyo kujipanga vizuri ili lengo hilo lifikiwe.

Alisema wafanyakazi wa Hazina ndiyo wanaobeba jukumu hilo wakati Serikali inajitahidi kupambana na mtikisiko wa kiuchumi hususan kipindi hiki cha kuelekea bajeti.Alisema Serikali imeomba nguvu ya kujiongezea uwezo kutoka mashirika ya kimataifa, nchi za Mashariki ya Kati na Asia.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, Ramadhan Khijjah alisema kuna tatizo la wafanyakazi wa wizara hiyo kuogopa kuzungumza katika vikao vya baraza hilo.

“Watu waoga huogopa kuzungumza. Wanawahofia wakuu wao wa idara jambo ambalo halijengi,” alisema.
Alisema hali hiyo inachangiwa na walio wengi kuogopa kuchukiwa na mabosi wao jambo ambalo alilipinga na kuwatoa hofu akiwataka wawe wazi.

Alisema mabaraza hayo ndiyo sehemu ya kukosoa, kuelekeza na kubainisha kasoro zilizopo ili hatua zichukuliwe na kujenga mshikamano kwa manufaa ya Taifa na jamii kwa ujumla.
 

Wabunge wakataa bajeti ya Wizara

               Makamo mwenyekiti(Hesabu za serikali za Mitaa)
                                             idd Azzan


Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii wamegoma kupitisha bajeti ya Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana kwa kuwa imeshindwa kutoa mchanganua wa bajeti ya mwaka uliopita.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Jenista Muhagama, alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi kuhusu suala hilo ambapo alisema kuwa wameshindwa kuipitisha bajeti ya wizara hiyo kwa kuwa haijaonyesha kiasi cha fedha ilichopewa na matumizi yake.

Alisema wizara hiyo ilitakiwa kutoa ufafanuzi sahihi kuhusu bajeti iliyopita ili Kamati iweze kuipitisha lakini imeshindwa kufanya hivyo.

Muhagama alisema waliipatia muda wa  kuonyesha ripoti ya mchanganua wa bajeti iliyopita na kwamba matumizi ya miradi ya maendeleo hazikuwekwa, hivyo Kamati haikuwa tayari kuipitisha bajeti hiyo.

Wakati huo huo, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Murtaza Magungu (CCM), ameitaka serikali kuipatia Bodi ya Mazao Mchanganyiko na Nafaka kiasi cha Sh bilioni 10 kama mtaji ili waweze kuingia katika ushindani wa biashara kwa lengo la kushusha gharama za vyakula.

Alisema bodi hiyo itakuwa inafanya kazi yake ya kununua chakula kwa wakulima na kuviuza kwa wananchi kwa gharama nafuu ili kushindana na wafanyabiashara katika kushusha bei za vyakula.

Magungu alisema endapo serikali ikishindwa kuweka ushindani katika biashara tatizo la mfumuko wa bei litaendelea kuwakabili wananchi.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za  Mtaa ( LAAC), Idd Azzan, ameagiza Mkaguzi wa Ndani wa Hesabu za Halimashauri ya Wilaya ya Nkasi kukatwa asilimia 15 ya mshahara wake wa mwezi huu kutokana na uzembe aliouonyesha.

Alisema hakuna mchanganuo wa fedha dhidi ya miradi mbalimbali iliyofanyika katika Halmashauri hiyo ambapo ilitakiwa ikaguliwe mahesabu yake.

"Hatutaki kuona figure tunahitaji kuona huo mchanganuo wa matumizi ya fedha yalivyofanyika ikifika Julai 8, muwe mmeshatupatia matumizi ya miradi hiyo kwani mahesabu yenu yana mikanganyiko," alisema.

Alisema Mkaguzi wa ndani anatakiwa kulisimamia suala hilo kwa umakini na kujua mchanganua ya fedha hizo za miradi zilivyotumika hivyo adhabu hiyo itamfanya asimamie shughuli zake kwa umakini.